Image
Image

Mchezaji wa muda mrefu Zimbabwe atimuliwa kwa kupanga matokeo ya mechi.

Chama cha kandanda nchini Zimbabwe (Zifa) kimemtimua mwanakamati Edzai Kasinauyo kutokana na madai kuwa alipanga matokeo ya mechi.
Bwana Kasinauyo analaumiwa kwa kushiriki katika kupanga mechi wakati wa michuono ya nchi hiyo ya kufuzu kwa mashindano ya taifa bingwa barani Afrika na Swaziland tarehe 25 mwezi Machi.
Taarifa kutoka (Zifa) zilisema kuwa uchunguzi unaendelea. Kasinauyo mwenye umri wa miaka 40 amekana madai hayo.
Yeye ni mchezaji wa zamani wa kiungo cha kati na aliwakilisha nchi yake katika mashindano wa kuwania kombe la taifa bingwa barani Afrika mwaka 2006.
Alichaguliwa kwenye kamati kuu ya Zifa mwezi Disemba.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment