Image
Image

UEFA yaipiga marufuku Galatasaray kutoshiriki mashindano yeyote kwa miaka miwili.



Klabu ya Uturuki Galatasaray imepigwa marufuku ya kutoshiriki mashindano yeyote yalioandaliwa na shirikisho la soka barani ulaya UEFA kwa kipindi cha miaka miwili kwa kukiuka kanuni za uadilifu wa kifedha
(financial fair play).
Mabingwa hao wa soka ya Uturuki walisajili hasara kubwa iliyolazimu UEFA kuchukua hatua baada ya ufichuzi mwezi Januari.
Galatasaray ilifuzu kwa hatua ya makundi katika kinyang'anyiro cha kuwania kombe la mabingwa barani Ulaya msimu uliopita.
Vigogo hao wa soka ya Uturuki wanashikilia nafasi ya 5 hivi sasa katika jedwali la ligi kuu.
Galatasaray, ambayo iliilaza Arsenal kupitia mikwaju ya penalti katika fainali za kuwania kombe la UEFA mwaka wa 2010 wamekuwa wakifuzu kwa mechi za kombe la mabingw barani ulaya katika misimu 4 mfululizo.
Msimu huu wanacheza katika ligi ya daraja la pili yaaani Europa ambapo waliambulia kichapo mikononi mwa Lazio.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment