Image
Image

Umoja wa Mataifa watoa wito wa kulinda raia wa Sudan Kusini.

Mjumbe maalum wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Bibi Ellen Margrethe Loj amerudia msimamo wa Umoja huo wa kuendelea kuwalinda raia nchini Sudan Kusini.
Bibi Margrethe ametoa wito kwa wadau wote nchini humo kujiepusha na vitendo au kauli zinazoweza kuchochea migogoro, na kuheshimu kanuni za Umoja wa Mataifa kama vile kutokuwa na silaha kwenye vituo vya Umoja huo.
Mwakilishi huyo aliyasema hayo wakati akitembelea eneo la Malakal kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kutathmini hali ilivyo na kukutana na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kijamii.
Watu wasiopungua 7 waliuawa mwezi uliopita na wengi kujeruhiwa wakati watu wasiojulikana waliposhambulia kituo cha Umoja wa Mataifa cha Malakal. Kituo hicho cha Malakal kinahifadhi raia 50,000 ambao wamekimbia makazi yao kutokana na vita.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment