Image
Image

Wanawake CCT waitaka Serikali kuchunguza biashara haramu ya kusafirisha binadamu


Umoja wa wanawake wa makanisa ya kikirsto Tanzania (CCT) katika wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga  wametoa tamko la pamoja kulaani biashara haramu ya kusafirisha binadamu ndani na nje ya nchi huku wakiitaka serikali kuchunguza chanzo cha biashara hiyo na kuwachukulia hatua kali za kisheriri watakaobainika kuhusika na biashara hiyo.
kauli hiyo imetolewa katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kanisa katoliki Parokia ya mtakatifu Theresia Segese Kahama huku wakidai kuwa waathirika wa kubwa wa biashara hiyo ni wanawake na watoto wakike wanaorubuniwa na kuuzwa kwa watu wasio na malengo mazuri.
Kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa kinamama wa CCT kahama Bi. Laurensia Gervas amesema mtandao wa wafanya biashara haramu ya binadamu imeanza kuota mizizi katika maeneo ya vijijini ambapo wanazirubuni familia masikini na watu wanaoishi katika mazingira magumu na kuwachukua watoto wakike kuwauza nje ya nchi.
Bi.Ester Shija ni mlezi wa wanawake kata ya Segese wilayani Kahama Shinyanga amewaasa wanawake wote nchini kulea familia zao kwa kuzingatia maadili ya upendo na kuweka misingi mizuri ya malezi huku akiwataka kuacha kutoa lugha chafu kwa wanaume hali ambayo inachangia kusanbaratisha ndoa na kusababisha mateso kwa watoto wadogo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment