WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Mh. Ummy Ally Mwalimu amepokea msaada wa fedha kwa ajili ya kuwezesha matibabu
ya wagonjwa wa moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo kwa
msaada huo, jumla ya watoto 101, wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo katika
taasisi hiyo kwa gharama za fedha hizo zilizotolewa na Jumuiya ya Kihindu
waishio Dar es Salaam ijulikanayo kama BAPS Charity, kwa kuguswa kwao na kutoa
msaada mkubwa na upendo waliouonyesha kwa watanzania wanaosumbuliwa na maradhi
ya moyo.
Wiziri Ummy amebainisha kuwa, kiasi cha msaada unaotolewa utawezesha wagonjwa wapato hao kupatiwa matibabu ya moyo hivyo kuwa, faraja kubwa kwa wagonjwa waliokuwa wakisubiria huduma hizo kwa muda mrefu kutokana na kushindwa gharama za matibabu yake.
Wiziri Ummy amebainisha kuwa, kiasi cha msaada unaotolewa utawezesha wagonjwa wapato hao kupatiwa matibabu ya moyo hivyo kuwa, faraja kubwa kwa wagonjwa waliokuwa wakisubiria huduma hizo kwa muda mrefu kutokana na kushindwa gharama za matibabu yake.

Aidha, kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH),
Profesa Mohamed Janabi amepongeza kwa msaada huo kwani utasaidia kutoa matibabu
kwa watoto hao 101, huku pia taaisi yake ikikabiliwa na changamoto ya wagonjwa
wengi ambapo amezitaka taasisi na wadau wengine kujitokeza kuchangia
ilikupunguza wagonjwa wanaosubiria kupatiwa matibabu hasa upasuaji.
Prof. Janabi ameeleza kuwa, matibabu ya wagonjwa wa moyo yana gharama kubwa kwani kwa mtoto mmoja ndani ya nchi yanafikia hadi Milioni nne (Mil 4) huku kwa nje ya nchi matibabu hayo yakifikia hadi Milioni 16, gharama hizo ni kubwa hivyo wadau na taasisi binafsi zimeombwa kujitokeza ilikuokoa maisha ya wagonjwa wengi hasa watoto ambao wapo katika taasisi hiyo na mikoa mingine.
Prof. Janabi ameeleza kuwa, matibabu ya wagonjwa wa moyo yana gharama kubwa kwani kwa mtoto mmoja ndani ya nchi yanafikia hadi Milioni nne (Mil 4) huku kwa nje ya nchi matibabu hayo yakifikia hadi Milioni 16, gharama hizo ni kubwa hivyo wadau na taasisi binafsi zimeombwa kujitokeza ilikuokoa maisha ya wagonjwa wengi hasa watoto ambao wapo katika taasisi hiyo na mikoa mingine.


0 comments:
Post a Comment