Image
Image

Zaidi ya 7 wapoteza Maisha wengine wajeruhiwa ajali ya Lori na Basi Matumbi.





Taharuki kubwa imetanda leo baada ya kutokea ajali iliyohusisha magari matatu na kupoteza maisha ya watu wa tatu na wengine 19 kujeruhiwa huku wengine hali zao zikielezwa kuwa Mbaya.
Mapema sakumi na moja za asubuhi kilisikika kishindo kikubwa barabarani mithili ya bunduki hali iliyolazimu raia kujitokeza kushuhudia hicho kishindo kilikuwa cha nini ndipo wakakuta ajali iliyo husisha magari hayo matatu.
Kwa mujibu wa Mashuhuda walidai kuwa watu waliopoteza maisha kutokana na ajali hiyo huenda wakazidi 10 kutokana na jinsi walivyokuwa wakiokoa waliona na hata kushuhudia hali mbaya zao zilizokuwa hazina matumaini ya uhai na wengine wakiwa wamejeruhiwa vibaya na gari likiwa limeharibika vibayaya.
Polisi wa ilala walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa Chanzo cha ajaki  ni Lori la Mchanga kuligonga basi la abiria aina ya DCM kwanyuma ndipo likayumba likapoteza muelekeo na kujikuta likimshinda dereva na kuruka upande wa pili wa bara bara ndipo likakutana uso kwa uso na Lori lililokuwa limebeba Ng’ombe likipeleka machinjio ya Vingunguti na hivyo kutokea kwa ajali.
Basi la Abiria lilikuwa likitokea Gongo la Mboto Ubungo DCM T 629 CRT huku likiwa linaongozana na Lori lamchanga T 277 DAU lililokuwa limeligonga kwa nyuma(Ubavuni) ndipo hapo sasa derweva wa DCM gari ikamshinda nguvu na likavuka upande wa pili likakutana na Lori T 109 DDX ambalo nalo lilikuwa lipo mwendo wa kasi likiwahi kupeleka Ng’ombe mnadani vingunguti likitokea njia ya Ubungo.
Mashuhuda waliokuwa hapo eneo la tukio ndio waliokuwa wakwanza kutoa msaada kwa majeruhi na na waliopoteza maisha kusaidiana na polisi kuwapandisha kwenye gari kusudi wawahishwe Hospitalini.
Mashuhuda waliokutwa na kamera yetu ya Tambarare Halisi waliduwaa kuangalia ajali hiyo huku wengine wakiishiwa hata nguvu kwa kuona ndugu na jamaa zao wakiwa katika hali mbaya baada ya ajali.
Wamesema kunahaja kwa madereva kuwa makini sana huku wakitupia lawama Lori la mchanga lililoonekana kutaka kulipita basi la abiria kusudi liwahi nahivyo kujikuta safari hiyo ikiishia Tabata Matumbi baada ya ajali kutokea.
Licha ya Polisi kufika eneo hilo wamesem,a kuwa kuna haja ya eneo hilo kuwekwa matuta kwani ajali zimekuwa ninyingi zikitokea eneo hilo si mchana wala usiku hivyo ipo haja uangaliwe utaratibu.
Hata hivyo kutokana na ajali hiyo foleni ilichukua takribani saa tatu ndipo msaada wa kuondolewa kwa gari hizo zilizopata ajali zikaanza eneo hilo.
Waliopoteza Maisha na Majeruhi inaelezwa wamehifadhiwa hospitali ya Muhimbili na wengine Amana jijini Dar es Salaam.
Tutaendelea kuwafahamisha kitakacho jiri zaidi.
ubavuni lilokuwa linatoka Buguruni kuelekea Ubungo na kisha basi hilo kupoteza muelekeo wa safari na kuruka upande wa pili wa barabara na kugongwa tena na lori lingine aina ya SCANIA lilokuwa limebeban ng’ombe waliokuwa wanapelekwa Machinjioni.Polisi wamethibitisha hilo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment