Image
Image

Familia yazika Maiti ya Kikristo kiislamu Upareni –Usangi Kilimanjaro.




Hii nayo imechukua nafasi katika Story za leo licha yakuwa mara kadhaa umekuwa ukisikia watu wakilalama kwamba wanafika hospitali kwaajili ya kuchukua miili ya ndugu zao waliofariki dunia na kukuta imebadilishwa na kupewa mtu mwingie lakini kwa hii ni tofauti kidogo,Ambapo familia moja iliyokuwa imefiwa na ndugu yao imejikuta imefika Hospitali ya Muhimbili kuchukua mwili wa ndugu yao Mochwari na kupewa mwili ambao ni wa familia nyingine ya Kikiristo na Kuzikwa Kiislam Usangi wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro na wakiislam kuachwa Mochwari ya Muhimbili.
Ningumu kuamini ila yabidi kuamini Mwili wa Bi.Janeth Teodory ambao ulikuwa umehifadhiwa Hospitali ya Muhimbili mara baada ya kufariki dunia siku ya Tarehe 8/04/2016  umekutwa umebadilishwa na kupewa familia nyingine iliyokuwa imekuja kuchukua mwili wa ndugu yao Bi.Amina Sudi aliyefariki Siku ya ijumaa usiku kuamkia jumamosi ya tarehe 8/4/2016 nakusafirishwa kupelekwa Mkoani Kilimanjaro kwaajili ya maziko yaliyokuwa yanafanyika Upareni - Usangi Wilyaya ya Mwanga Mkoa wa Kilimanjaro.
Baada ya miili hiyo kuchanganywa katika sakata hilo siku ya jumapili tarehe tisa majira ya saa saba mchana taratibu zote ziliweza kufanyika kwaajili ya familia hiyo ya Sudi kumuhifadhi waliye amini ni mama yao Bi.Amina Sudi huko upareni huku watu wakilia na huzuni kedekede kwa kujua mpendwa wao huyo ndiye katolewa jijini Dar es Salaam kwaajili ya maziko.
Kwakuwa Marehemu Amina Sudi alikuwa ni Muislamu basi taratibu za kuaga hazikuweza kufanyika kama wafanyavyo wakristo kwamba kuna muda wa kuaga ambao wakati mwingine huchukua hata siku mbili na yatatu kuzika lakini kwa maiti hiyo ya kiislam ilikuwa ni bandika bandua ambapo hadi wanakwenda makaburini kuzika bado kulikuwa hakuna utambuzi wa kutosha kuwa wanaye mzika si ndugu yao wamechanganya mambo.
Baada ya shughuli hiyo ya Maziko kumalizika kila mmoja wao alirudi kutoka makaburini na kurudi nyumbani palipo na msiba na kusikiliza kilichokuwa kikiendelea haswa kwa waislam upo ujumbe ambao pia shehe huutoa kwa watu wote waliohudhuria msiba huo ili wakumbuke kwamba dunia ni mapito tu na huko ndiko tuendako nashughuli hiyo ikafanyika ikamalizika nawatu kutawanyika hivyo siku ya jumatatu Tarehe kumi ilitazamiwa kuwa patafanyika duwa maalumu ya kumuombea Marehemu kabla ya watu wote haswa wanandugu kutawanyika kuelekea wanapo fanyia kazi na kujipatia riziki za siku.
  Ndugu wa Marehemu Janeth.
Katika Hospital ya Taifa Muhimbili ndugu wa Marehemu Bi.Janneth Teodory walifika Asubuhi na Mapema kuweza kufanya Taratibu za kuchukua Mwili wa Mpendwa wao ili waende wakampumzishe huku wakiwa tayari wamenunua Sanduku la kuhifadhia ndugu yao huyo huku watu huko majumbani wakiwa katika huzuni ya kusubiri mpendwa wao kwamba sasa analetwa ili taratibu zikamilike za lini watakwenda kumuhifadhi lakini mambo yakawa tofauti.
Baada ya Kufika Muhimbili sasa hiyo jana tarehe 10/4/2016 na kuulizia Mwili wa mpendwa wao waliibngia ndani na kuoneshwa miili yliyokuwapo lakini wao hawakujua lolote kwamba kuna kuna mkanganyiko wa mambo umejitokeza,katika tafuta tafuta waliukosa mwili wa mpendwa wao jambo lililo wafanya kupigwa na butwaa kwa mpendwa yetu kaenda wapi ama imekuwaje na mawazo kuwapelekea kwamba huenda kaibiwa.
Sasa baada ya sintofahamu hiyo kujitokeza hiyo asubuhi basi ikabidi kujua ilikuwaje ambapo kwa wanaohusika nan a Mochwari wakiwamo wasimamizi ilibidi kuangalia tena ndipo kugundua kwamba walichanganya mambo na kukuta kwamba Mpendwa wao kasafirishwa kwenda kuzikwa Usangi huko Upareni tena Kiislam wakati ni Mkristo,na Maiti ya Kiislam kuachwa Dar es Salaam hali ambayo nawao wasingetazama vyema huenda wangeenda kuizika Kikiristo.
Baada ya kugundua hivyo Basi familia iliyo pewa mwili wa Marehemu Janneth kimakosa waliarifiwa hali iliyowafanya kupigwa na butwaa kwa kilichotokea huku wengine wakistyajabu kwakuwa kwao imekuwa nikama story tu kuzisikia kwa wengine lakini kwao haikuwahi kutokea.
Taarifa mara baada ya kuwafikia ilibidi tena taratibu kuanza upya kwa namna ya kuja kuchukua ndugu yao aliyeachwa huku Mochwari ya Muhimbili lakini kwa Taratibu maalumu huku Mwili wa Marehemu Janneth ukiwa umezikwa kiislam tayari huko Usangi.
Mpaka usiku wa tarehe 11/04/2016 Taratibu zilikamilika kwa kupewa vibali maalumu na Polisi huku hospitali ikitoa gari kwaajili ya kupeleka Mwili uliokosewa huko Usangi – Upareni na Uliozikwa Kufukuliwa na kurudishwa Dar es Salaam ili ndugu wenye mpendwa wao kuanza Taratibu upya za Mazishi kisha Maziko.
Tarehe yaleo 12/04/2016,Maziko ya Marehemu Amina Sudi wa Usangi yanafanyika Tena upya huku Mwili wa Marehemu Janneth Uliozikwa Kiislamu ukifukuliwa ili kurejeshwa Dar es Salaam na kukabidhiwa ndugu na Jamaa zao.
Kauli ya Mtoto wa Marehemu Janneth Teodory anasema kuwa Marehemu alikuwa anasumbuliwa na tumbo pamoja na figo,ambapo alifariki dunia katika Hospitali ya Muhimbili Tarehe 8/04/2016 na kwamba Tarehe 11/04/2016 walivyofika Muhimbili walikuwa tayari wamekamilisha taratibu zote za kuuchukua mwili huo kwa ajili ya Mazishi ya Mama yao Mpendwa lakini ndipo wakakutana na hali hiyo ya utofauti.
Kwa wakati Mwingine ndugu wa Marehemu Janneth walihoji kuwa yawezekana vipi ndugu kuuchukua Mwili ambao sio wao na wakajiridhisha ni ndugu yao na wakazika?
Ilikuwaje naye msimamizi wa Mochwari kutoa ndugu ambaye sio wa wahusika huku wakiwa na alama maalumu mara baada ya kufariki?.
Maswali hayo yalionekana niyautata kwa namna moja ama nyingine lakini nijambo ambalo limejitokeza na hakuna jinsi kikubwa nikuchukuliwa Mwili wa Mpendwa wao na kurudishwa.
Wakati wa ufuatiliaji ilibainika kuwa Marehemu hao wawili Janneth na Amina Sudi mafaili yao yalichanganywa na wahusika wa Mochwari ambapo hadi dakika za mwisho Process zote zinafanyika kwa Janneth zikijulikana kuwa ni Amina hali iliyokuwa niyakushangaza na wakati mwingine kuhoji umakini wa wasimamizi wa Mochwari na hata wahusika wanaiochukua miili yao.
Si leo kusikia miili ikichanganya lahasha ishaa tokea Mwanza,Tanga na  Amana jijini Dar es Salaam kwa siku za usoni hapa lakini imekuwa Tofauti kwa Mwili wa Kikristo kuzikwa Kiislam ndipo hapo kumeshangaza ulimwengu na hata ndugu na jamaa wa Pande Zote.
Kuzungumzia hili na kutaka kujua nikani haya yanajitokeza katika uchukuaji wa Miili ya Marehemu katika hospitali mbalimbali nchini Tambarare Halisi Ilibisha Hodi kwa uongozi wa Muhimbili lakini hapakuwa na Mafanikio ambapo Mkurugenzi wake wa hospitali ya Muhimbili alielezwa kuwa nje ya Ofisi, licha ya kukiri kutokea tatizo hilo la kutoa maiti kimakosa.
Msimamizi wa Mochwari alijaribu kuztaka kuzungumzia hali ilivyokuwa lakini aliacha kuzungumza pengine kwa kuhofia kibarua chake na kudai yeye si mzungumzaji wapo wazungumzaji na hivyo hali ya sinto fahamu ikaendelea kugubika vichwa vya Ndugu na Jamaa kwa kilichotokea.
Mwili wa Marehemu Janneth unatazamiwa kuletwa leo baada ya kufukuliwa huko Usangi – Upareni ulipokuwa umezikwa kimakosa tokea jumapili tarehe 9/04/2016 ambaopo ikiwa hadi hivi leo tarehe 12/04/2016 ni siku ya Tatu.
Ipo haja pia ya umakini kuwepo wakati wa utambuzi wa miili ya wapendwa walio fiwa ili kujua bndiye ama siye ili kuepusha minong’ono na maswali juu ya hili,na Pia wasimamizi katika Mochwari za Hospitali za Tanzania kuwa na Umakini wakuacha kuchanganya Mafaili ama kuwapiga danadana watu wanaokuja kuchukua chochote kitu kama baadhi ya wanaokutwa na mikasa hiyo kusema hali inayokuwaga humo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment