Image
Image

Moto wateketeza Mabweni mawili ya wavulana Tabora.


Hali ya taharuki imetokea katika shule ya Mtakatifu Petro iliyopo Manispaa ya Tabora baada ya Mabweni mawili kuteketea kwa moto wakati wanafunzi zaidi ya 138 wakiwa darasani.
Inaelezwa kuwa Moto huo ulizuka gafla tu ambapo sababu za kuzuka kwake hazikufahamika mara moja nahivyo kuunguza mabweni ya wavulana katika shule hiyo iliyokuwa imejengwa kwa zaidi ya Milioni 70.
Vitu vya wanafunzi vimeshindwa kuokolewa mara baada ya baada ya gari la zimamoto kuzama eneo la shule hiyo kutokana na ubovu wa Miundo Mbinu.
Kwa upande wa mkuu wa shule hiyo Bw.Simon Piter Kyalla akizungumzia sababu za kuzuka kwa moto huo shuleni hapo amesema hajafahamu mara moja kwani wao wameona tu moto ukiwaka hivyo kukumbusha moja ya tukio lilowahi kutokea Mwaka jana 2015 ambapo Mabweni mawili moja la wavulana,na la wasichana kwa nyakati tofauti yaliteketea kwa moto, akidai kuwa ni umeme.
Kufuatia tukio hilo la mabweni kuwaka moto katika mazingira ya kutatanisha tena mchana kweupe, mkuu wa wilaya ya tabora mjini bw, suleimani kumchaya ameamua kuifunfa shule hiyo kwa mda usiojulikana akidai kuwa, mpaka viongozi wa taasisisi hiyo wajihoji, akidai si kila simu ni tatizo la umeme .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment