Image
Image

Maalim:Vigogo wa Serikali ya SMZ watorosha fedha kwenda nje ya Nchi na wengine kununua Majumba.


Baada ya kuwa na Msigano kwa muda sasa visiwani Zanzibar kati ya vyama vilivyo na nguvu kikiwamo cha CUF na CCM mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 Mwaka jana kufutwa na Mwenyekiti wa Uchaguzi na hivyo uchaguzi huo kurudiwa Machi 20 2016 na CUF kususia Uchaguzi huo hatimaye jipu latumbuliwa.
Aliyekuwa mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad ameamua kutumbua jipu ndani ya Serikali ya Zanzibar baada ya kudai fedha nyingi zilitoroshwa kabla ya uchaguzi na vigogo wengi wa SMZ wana miliki fedha nje.
Maalim Seif Sharrif Hamad ametoa kauli hiyo visiwani Zanzibar wakati akiongea na waandishi habari kuelezea mikakati ya Chama cha Wananchi CUF katika kudai haki ya wananchi wa Zanzibar ambapo amesema kabla ya uchaguzi baadhi ya viongozi walisafirisha fedha nje ya nchi na wengine kununua majumba kwa fedha za umma ingawa hakuwataja viongozi hao.
Hatua ambazo CUF imezipanga kuchukua  maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF amesisitiza kuwa njia kubwa itaendelea kuwa ya amani na sio fujo wala vurugu ikiwa ni pamoja na kufuata utaratibu wa kwenda mahakama za kimataifa ingawa zina utaratibu wake lakini tayari baadhi ya taasisi za haki za binaadamu wameanza kulishughulikia suala la uvunjaaji wa haki hizo.
Huu ni mkutano wa pili wa CUF kufanya kuelezea msimamo wao wa kutoitambua Serikali ya Dk.Ali Mohamed Shein na harakati wanazozichukua  ili kuhakikisha  mamauzi ya wananchi ya Ockoba mwaka jana yanaheshimiwa na kutendeka.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment