Image
Image

MCT yatangaza majina ya wateule wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2015.


•Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora,Tom Nyanduga kuwa Mgeni Rasmi
Kamati ya maandalizi ya EJAT 2015 leo limetangaza majina 84 ya wateule wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2015. Idadi hiyo ni ongezeko la wateule 31 ukilinganisha na tuzo za 2014 ambapo wateule walikuwa ni 53 tu.
Pia kamati imeeleza kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tom Bahame Nyanduga ndio Mgeni Rasmi kwenye Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT ) 2015  zitakazofanyika kwenye tamasha la usiku la utoaji wa tuzo hizo  Aprili 29, 2016 , Dar es Salaam.
Kutangazwa kwa wateule wa EJAT 2015 kunafuatia kukamilika kwa kazi ya kuzipitia na kuchagua zile zilizo na ubora zaidi iliyofanywa na jopo la majaji 10 lililokaa mwezi Machi mwaka huu. Majaji hao ambao ni wataalamu mbalimbali wa masuala ya habari walipitia kazi za kiandishi zaidi ya 570 zilizowasilishwa kwenye makundi ya kushindaniwa 22 kwenye tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2015.
Ripoti ya jopo la majaji hao kuhusu wateule wa EJAT 2015, inaonyesha kuwa  kumekuwa  na ongezeko kubwa kwa  wateule kwa upande wa luninga ambapo kuna wateule  27 kutoka wateule wawili katika tuzo za 2014. Pia kuna ongezeko kwenye wateule wa redio kutoka 17 hadi 27. Hata hivyo kwa upande wa magazeti wateule wamepungua kidogo kutoka wateule 34 wa tuzo za 2014 hadi 32 kwa tuzo za mwaka 2015. 
Idadi ya wateule wanawake pia imeongezeka kufikia 28 kutoka wateule 18 kwenye tuzo za EJAT 2014.  Pia ripoti inaonyesha kuongezeka kwa kazi zilizoletwa na redio za kijamii mwaka huu ambapo baadhi yao zimeweza kutoa wateule kwenye tuzo za EJAT 2015.
Jopo hilo la majaji liliongozwa na mwenyekiti wake, Bi. Valerie Msoka, wajumbe wengine walikuwa  Dk. Joyce Bazira Ntobi ambaye alikuwa katibu wa jopo, na Ali  Uki. Wanajopo wengine walikuwa Jesse  Kwayu, Kiondo Mshana,  Juma Dihule, Godfrey  Nago, Nathan Mpangala na  Pili Mtambalike. Waandishi hao 84 wataingia kwenye kinyang’anyiro cha mashindano ya EJAT 2015. 
Majaji hao 10 waliapishwa na Rais wa Baraza la Habari Tanzania, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Machi  11, 2016 kabla ya kuanza kazi hiyo. Hii itakuwa ni  mara ya saba kuwatuza waandishi waliofanya vizuri katika kazi zao za kiuandishi chini ya utaratibu wa EJAT.
Sambamba na EJAT, Jopo la wataalam kwa ajili ya Tuzo ya Maisha ya Mafanikio katika Uandishi wa Habari (LAJA) umeanza kazi ya kutafuta mteule wa tuzo hiyo kwa mwaka huu ambae atatangazwa wakati wa Tamasha hilo la usiku.  Jopo la LAJA linalongozwa na Mwenyekiti wake Bi. Lilian Kallaghe lina wajumbe watano ambao ni pamoja na Hamis Mzee, Fili Karashani, Joseph Kulangwa na Wenceslaus Mushi.
Makundi yaliyoshindaniwa ni yafuatayo:
1. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Uchumi na Biashara
2. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Michezo na Utamaduni
3. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Mazingira
4. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Afya
5. Tuzo ya Uandishi wa Habari za VVU/Ukimwi
6. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Watoto
7. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Utawala Bora
8. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Jinsia
9. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Sayansi na Teknolojia
10 Tuzo ya Uandishi wa Habari za Uchunguzi
11. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Afya ya Mama na Mtoto
12. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Elimu
13. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Utalii na Uhifadhi
14. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Watu Wenye Ulemavu
15. Mpiga Picha Bora – Magazeti
16. Mpiga Picha Bora – Runinga
17. Mchora Katuni Bora
18. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Kilimo
19. Tuzo ya Afya ya Uzazi kwa vijana
20. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Gesi, Mafuta na Uchimbaji Madini
21. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Manunuzi ya Umma
22. Tuzo ya Uandishi wa Habari za Kodi na Ukusanyaji Mapato
Ifuatayo ni orodha ya wateule wa EJAT 2015 ambao wanatoka kwenye vyombo mbalimbali vya habari

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment