Image
Image

Waziri mkuu wa uingereza David Cameron atangaza mapato yake ya miaka 6 iliyopita.



Waziri mkuu wa uingereza,David Cameron, ametangaza takwimu za mapato yake na kodi aliyotozwa katika kipindi cha miaka 6 iliyopita kufuatia kashfa ya nyaraka za panama.
Ni mara ya kwanza kwa waziri mkuu aliyeko madarakani kufanya hivyo nchini uingereza..
Waziri mkuu  Cameroon amekuwa akikosolewa tangu nyaraka hizo za siri kufichuka kutoka panama zinazoeleza kuwa baba yake alianzisha wakfu na kampuni ya hewa nchini panama.
Alikiri kuwa aliuza hisa kadhaa za wakfu huo na kupata dola za marekani $44,000 kabla kuchaguliwa kuwa waziri mkuu.
Takwimu hizo zinaonyesha kuwa cameron alipokea jumla ya dola 300,000 za marekani kutoka kwa mama yake mwaka 2011, muda mfupi baada ya yeye kurithi dola 44,000 kutoka kwa baba yake.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment