Image
Image

Serikali ya Gambia yapiga marufuku muziki na densi katika mwezi wa Ramadhan.

Serikali ya Gambia imetangaza marufuku ya kupiga muziki na kucheza densi kwenye migahawa ya burudani katika mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Idara ya polisi nchini humo pia imetoa onyo kali kwa wananchi kutokiuka sheria hiyo iliyozuia muziki na densi mchana na usiku kwa kipindi cha mwezi mzima.
Mkuu wa polisi pia amewataka wananchi kuweka ushirikiano katika suala hilo na kuripoti kesi yoyote ya ukiukaji wa sheria hiyo.
Mnamo mwezi Desemba mwaka 2015, rais Yahya Jammeh alitangaza rasmi Gambia kuwa taifa la Kiislamu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment