Image
Image

TFF yambonyeza kizenji Jerry Muro kwa mwaka mmoja kutojihusisha na soka.

MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Yanga, Jerry Muro (pichani) amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka na kulipa faini .
Kwa mujibu wa televisheni ya Ch
annel 10, Muro alifungiwa baada ya kikao kilichofanyika jana.
Taarifa nyingine ambazo zilipatikana muda mchache zilisema kuwa Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jana ilichukua hatua hiyo baada ya kikao kirefu.
Habari hizo zilizopatikana jana usiku zilisema Muro alifungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka baada ya kupatikana na hatia ya kuipinga na kuishambulia TFF kwenye vyombo vya habari. Kikao cha Kamati ya Maadili ya TFF, kilikaa jana bila ya Muro kuwepo kwa kuwa wakati mwaliko unatoka alikuwa nje ya Dar es Salaam.
Awali, Muro alisema alikuwa mapumzikoni Machame mkoani Kilimanjaro.
Hatahivyo, msemaji wa TFF, Alfred Lucas alisema jana saa 1:50 usiku kuwa kikao hicho kilikuwa kikiendelea na alishangaa taarifa hizo zilipatikana wapi.
“Na mimi kuna watu wamenipigia wamesema kuna taarifa katika mitandao inasema Jerry kafungiwa, sijui wamezitoa wapi kwani na mimi niko hapa nje na kikao kinaendelea, lakini taarifa kamili kesho saa nne asubuhi”, alisema Lucas.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment