MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Yanga, Jerry Muro (pichani) amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka na kulipa faini .
Kwa mujibu wa televisheni ya Channel 10, Muro alifungiwa baada ya kikao kilichofanyika jana.
Taarifa
nyingine ambazo zilipatikana muda mchache zilisema kuwa Kamati ya
Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jana ilichukua hatua hiyo
baada ya kikao kirefu.
Habari hizo zilizopatikana jana usiku zilisema
Muro alifungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka baada ya
kupatikana na hatia ya kuipinga na kuishambulia TFF kwenye vyombo vya habari. Kikao cha Kamati ya Maadili ya TFF, kilikaa jana bila ya Muro kuwepo kwa kuwa wakati mwaliko unatoka alikuwa nje ya Dar es Salaam.
Awali, Muro alisema alikuwa mapumzikoni Machame mkoani Kilimanjaro.
Hatahivyo,
msemaji wa TFF, Alfred Lucas alisema jana saa 1:50 usiku kuwa kikao
hicho kilikuwa kikiendelea na alishangaa taarifa hizo zilipatikana wapi.
“Na mimi kuna watu wamenipigia wamesema kuna taarifa katika mitandao inasema Jerry kafungiwa,
sijui wamezitoa wapi kwani na mimi niko hapa nje na kikao kinaendelea,
lakini taarifa kamili kesho saa nne asubuhi”, alisema Lucas.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment