Image
Image

Waziri Mkuu wa Italia atembelea eneo ambako treni mbili za abiria zimegongana.

Waziri Mkuu wa Italia,MATTEO RENZI,ametembelea eneo ambako treni mbili za abiria zimegongana uso kwa uso na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 27 na wengine  wamejeruhiwa baadhi yao hali zao ni mbaya.
Waziri Mkuu RENZI amewahimiza wananchi  wa Italia kutoa damu kuwasaidia majeruhi wa ajali hiyo.
Waziri Mkuu huyo wa Italia ameagiza maafisa wa nchi hiyo kuchunguza kubaini nini chanzo cha kutokea kwa ajali hiyo.
Treni hizo zilikuwa kwenye n
jia moja kati ya Miji ya Bari na Barletta na haijafahamika nini kilisababisha ajali hiyo wakati hali ya hewa ilikuwa nzuri katika Mkoa mzima wa Puglia.
Waokoaji kutoka Idara ya Dharura walifika na kuwaokoa abria kutoka kwenye mabehewa yaliyojikunja na kuharibika vibaya na kufanikiwa kumtoa mtoto mchanga akiwa hai na kukimbizwa hospitali.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment