Kiongozi
wa upinzani Hakainde Hichilema anawasilisha kesi katika Mahakama ya
Kikatiba kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu yalimyompa ushindi rais Edgar
Lungu.
Tume ya Uchaguzi mapema wiki hii ilimtangaza Lungu mshindi kwa
kupata asilimia 50.35 ya kura zote zilizopigwa wiki iliyopita huku
mpinzani wake akiwa wa pili kwa kupata asilimia 47.63 ya kura.
Wiki
hii, Polisi iliwakamata zaidi ya wafuasi 150 wa upinzani katika mji wa
utalii wa Livingstone Kusini mwa nchi hiyo; waliokuwa wanaandamana
kupinga ushindi wa rais Lungu.
Kiongozi huyo wa upinzani anataka
Mahakama hiyo kutupilia mbali matokeo hayo kwa madai ya kuwepo kwa wizi
wa kura hasa jijini Lusaka.
Kuanza kwa kesi hii kutamaanisha
kusitishwa kwa sherehe za kumwampisha rais Lungu zilizotarajiwa
kufanyika hivi karibuni, hadi kesi hiyo itakapoamuliwa baada ya siku 14.
Wakati
wa kampeni za kisiasa, Hichilema aliwaambia wafuasi wake kuwa atakwenda
Mahakamani kupinga matokeo ikiwa Lungu atatangazwa mshindi, na alikuwa
na uhakika wa kushinda.
Wachambuzi wa siasa nchini humo wanaonya kuwa
ikiwa Mahakama itaamua kutupilia mbali matokeo hayo, wafuasi wa rais
Lungu hawatakubali uamuzi huo kutokana na kauli hiyo ya Hichilema.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment