Majaribio matatu ya chanjo kwa mnyama aina ya Tumbili yameonyesha kuzaa matunda .
Majaribio
hayo ya chanjo hiyo yalifanyiwa kwa Tumbili watatu na mtaalamu wa afya
Dk Dan Barouch katika kituo cha afya cha Beth Israel Deaconess
kilichoko nchini Marekani.
Ripoti ya matokeo ya chanjo hiyo
ilitolewa katika jarida la sayansi na kufahamisha kuwa chanjo hiyo
itaweza kutumika kwa binadamu mwaka 2017.
Kwa mujibu wa takwimu
zilizotolewa ni kwamba raia zaidi ya 650,000 kutoka Marekani waliokuwa
wanasafiri kwenda mataifa mengine walipatikana na virusi hivyo vya Zika .
Shirika
la Afya la Dunia (WHO)pia lilitoa ripoti mnamo Julai 27 iliyoonyesha
kuwa virusi vya Zika vilipatikana katika mataifa 67 .
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment