Image
Image

Kenya yasema ipo tayari kuisaidia kiuchumi Sudani Kusini kufuatia mgogoro wa Kisiasa.

Serikali ya Kenya imesema iko tayari kuisaidia Sudan Kusini kukabiliana na changamoto za kiuchumi zilizosababishwa na mgogoro wa kisiasa.
Msemaji wa ikulu ya nchi hiyo Manoah Esipisu amesema, hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo kati ya rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na ujumbe wa Sudan Kusini uliokuwa ziarani nchini Kenya, na kusema lengo la mkutano huo lilikuwa ni kuomba msaada wa Kenya.
Wakati huohuo, China imeahidi kutoa dola za kimarekani milioni 10 ili kuisaidia Sudan Kusini kukabiliana na mahitaji ya kibinadamu. Balozi wa China nchini humo Ma Qiang amesema, fedha hizo zitatumika kununua chakula na mahitaji mengine, ikiwa ni juhudi za kuokoa maisha ya maelfu ya watu walio kwenye hali mbaya ya kibinadamu.
Habari nyingine zinasema, makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini Taban Deng, amewasili nchini Sudan jana kwa ziara ya kiserikali. Deng alifanya mazungumzo na makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Bakri Hassan Saleh hapo jana, na hii leo anatarajiwa kukutana na rais Omar al-Bashir wa Sudan.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment