Image
Image

Serikali yaanza kutekeleza azma ya Rais Magufuli ya Tanzania ya Viwanda Morogoro.

 Na.DevothaSongorwa,Morogoro 
...............................................................................................................................
Serikali mkoani Morogoro imesema inaendelea na shughuli za ujenzi na uboreshaji viwanda ili kutimiza ahadi iliyotolewa wakati wa kampeni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk. JOHN POMBE MAGUFULI kuifanya nchi kuwa ya viwanda.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk. KEBWE STEPHEN KEBWE wakati akizungumza na wananchi kwenye uwanja wa jamhuri  ambapo amesema kuwa  serikali imetenga eneo la Mkonge lililopo Tungi kujengwa viwanda na makazi.
Ameongeza kuwa maeneo ya Mazava  serikali inatarajia kujenga kiwanda kitakachochakata nguo za michezo na wanatarajia kutoa ajira kwa zaidi ya watu 7000, ili kupunguza janga la umaskini,  ukosefu wa ajira na kuliongezea  pato taifa.
Aidha  Mkuu wa mkoa huyo Dk. KEBWE amesema  serikali ina mpango wa kuendeleza kilimo kuwa chenye tija, kumaliza ujenzi wa shule za sekondari, maabara, zahanati na nyumba za walimu, matumizi bora ya ardhi kwa taifa ili kumaliza mgogoro uliopo kwenye wilaya mbalimbali ikiwemo Mvomero, Kilombero, Malinyi, na Ulanga pamoja na kusimamia uhifadhi wa vyanzo vya maji  kuepukana na changamoto ya maji mkoani  Morogoro.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment