Image
Image

UN yaanzisha uchunguzi kubaini walinda amani wake walishindwa kulinda raia.

Jenerali mstaafu kwenye jeshi la Uholanzi ataongoza jopo huru la uchunguzi kubaini ikiwa walinda amani wa umoja wa Mataifa walishindwa kuwalinda raia wakati wa mapigano makali yaliyozuka kusini mwa mji mkuu wa Sudan Kusini, mwezi uliopita.
Meja jenerali Patrick Cammaert atawasilisha ripoti ya uchunguzi huo ndani ya mwezi mmoja kwa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ambapo matokeo yake yatawekwa wazi kwa uma, amesema msemaji wa umoja wa Mataifa.
Vikosi vya umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini vimejikuta kwenye shinikizo kubwa vikikosolewa kwa madai kuwa vilishindwa kuwalinda raia wakiwemo wanawake na wasichana ambao walibakwa jirani kabisa na kambi ya vikosi hivyo kwenye mapigano ya mwezi Julai mjini Juba.
Umoja wa Mataifa unasema kuwa umerekodi visa zaidi ya 200 vya ubakaji vilivyotekelezwa mwezi Julai peke yake na wanajeshi wa Serikali ambao ni watiifu kwa Serikali ya Rais Salva Kiir.
Mwezi uliopita, katibu mkuu Ban Ki Moon alitangaza kuwa ataanzisha uchunguzi huru kuhusu taarifa za walinda amani hao kushindwa kufika kwa wakati kuwasaidia raia waliohitaji msaada wakati wa mapigano na pia kuchunguza mashambulizi tofauti kwenye hoteli moja mjini Juba.
Wanajeshi wa Sudan Kusini wanatuhumiwa kuwabaka wanawake, kuwadhalilisha wafanyakazi wa umoja wa Mataifa na kumoiga risasi mwandishi wa habari kwenye shambulio la Julai 11 kwenye hoteli ya Terrain mjini Juba, ambapo walinda amani hao wanadaiwa kushindwa kufika kutoa msaada.
Uchunguzi huo utabaini ikiwa walinda amani wa umoja wa Mataifa walioko nchini Sudan Kusini wanaofahamika kama UNMISS, walidhibiti hali kimaadili na kuwalinda raia kwa muda muafaka, alisema msemaji wa umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment