Na.DevothaSongorwa,Morogoro
............................................................................................................................................................
Viongozi
wa dini zote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali wamefanya
Kongamamno la kuombea Amani Taifa la Tanzania ambalo limefanyika
mwishoni mwa wiki kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Akizungumza
na wananchi Mkuu wa mkoa wa Morogoro ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi
Dk KEBWE STEPHEN KEBWE amesema kuwa amani ni ya muhimu katika nchi ili
kuwepo kwa usalama wa wananchi na mali zao hivyo ni jukumu la kila
mwamnachi bila ubaguzi kujali na kudumisha amani iliyopo.
Amewataka
viongozi na watendaji wote wa serikali kuunda kamati ya Amani katika
maeneo yao jambo litakalosaidia kutoa elimu na kuhamasisisha jamii
kuachana na vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani ya nchi.
Aidha
Dk. KEBWE amewaonya wale wanaotarajia kufanya maandamano mnamo
september mosi mwaka huu kufuatia operesheni UKUTA inayoendeshwa na
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kuacha kufanya hivyo na badala yake
wafanye shughuli za kujieletea maendeleo.
Hata hivyo amewaomba
wananchi kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa za mtu yeyote
ambae wana mashaka nae na kuonyesha viashiria vya uvunjifu wa amani na
amewashukuru
Viongozi wa dini na madhehebu yote mkoani Morogoro kwa kushirikiana na serikali kuiombea amani nchi.
Ameitaka
Kamati ya Amani mkoani Morogoro kushirikiana na viongozi wa dini zote
kuendelea kutoa elimu kwa jamii kutambua kuwa amani ni msingi wa
maendeleo ya taifa na dunia kwa ujumla.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment