Image
Image

Majaji wa Kenya wapinga suala la marufuku ya vazi la hijab.

Majaji wa Kenya wamepinga suala la marufuku ya vazi la hijab nchini na kuunga mkono uhuru wa dini kwa wananchi wote.
Majaji hao pia wamemhimiza waziri wa elimu kushauriana na viongozi wa taasisi za taalum ili kuhakikisha uhuru na haki ya dini haikiukwi wala ubaguzi kutokea.
Jopo la majaji lililoongozwa na mwanasheria Phillip Waki wa mahakama kuu ya rufaa, lilifutilia mbali pendekezo la kuweka marufuku ya vazi la hijab hasa mashuleni.
Majaji hao pia walitoa wito kwa walimu kutofanya ubaguzi wa aina yoyote dhidi ya wanafunzi kwa misingi ya mavazi yao wala imani zao za kidini.
Kwa upande mwengine, Kadhi Mkuu wa Kenya Hammad Mohammed Kassim alitoa maelezo na kusisitiza kwamba vazi la hijab ni mojawapo ya masharti kwa wanawake wa Kiislamu.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment