Image
Image

Chama cha Msalaba mwekundu nchini kimeanza kuchukua hatua kukabiliana na ugonjwa wa kuharisha uliowakumba waomba hifadhi katika kijiji cha Kagunga.



Shirik isho  la  Chama cha  Msalaba mwekundu nchini limeanza kuchukua hatua kukabiliana na ugonjwa wa kuharisha uliowakumba waomba hifadhi katika kijiji cha Kagunga,Wilayani Kigoma kwa kupeleka huduma mbalimbali za jamii.
Meneja wa  shirikisho hilo  Mkoani Kigoma,JANE CHAGIE amesema  tayari timu ya watendaji  wameshakwenda  Kijijini Kagunga wakiwa na mahema kwa ajili ya waomba hifadhi hao kujihifadhi, dawa ya  kusafisha maji  pamoja  na watu wanaoshughulikia uchimbaji vyoo.
Akizungumzia suala la uchimbaji vyoo amesema,wamekabiliwa na tatizo kubwa la mahali pa kuchimba vyoo kutokana na sehemu kubwa ya eneo kuwa la Milima yenye mawe  na  idadi kubwa ya watu ikiwa kandokando ya Ziwa Tanganyika.
Kijiji cha Kagunga kinakadiriwa kuwa na zaidi ya waomba hifadhi Elfu -90  wanaosubiri kusafirishwa kwenda kambi ya wakimbizi Mtabila Wilayani Kasulu, hali inayosababisha uchafuzi wa mazingira katika kijiji hicho kutokana na huduma duni za afya na  jamii.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment