Image
Image

VITENDO VYA UJANGILI VYAENDELEA KUKITHIRI PORI LA SELOU MKOANI RUVUMA'


Na.Emmanuel Msigwa , Tunduru

Wimbi la vitendo vya ujangili dhidi ya Tembo katika Pori la Selou la Tunduru Mkoani Ruvuma ambalo limekithiri siku za hivi karibuni limesababisha tembo wengi kukimbia kwenye makao yao msituni na kwenda kwenye makazi ya watu na kusababisha maafa mbalimbali wilayani humo ikiwemo ya kushambulia mashamba ya mazao na kuua watu wawili.
Tembo
Zaidi ya ekari 25 za mazao mbalimbali ikiwemo mahindi ya wananchi katika vijiji vya Machemba, Misechera na Nakapanya zimeshambuliwa vibaya na Tembo huku tembo hao hao wakiua watu wawili katika kijiji cha Matemanga na Teleweni-Mlingoti wilayani Tunduru yote hiyo ikisababishwa kutokana na tembo hao kukimbia kwenye maeneo yao na kuja kwenye makazi ya watu kutokana na vitendo vya ujangili.

Kutokana na maafa hayo Mkuu wa wilaya ya Tunduru, CHANDE NALICHO akaongoza kikosi cha askari wa wanyapori pamoja na wananchi kuendesha zoezi la kufukuza Tembo hao katika maeneo yaliyoathiriwa huku akiwatoa wasiwasi wananchi kwamba Serikali imejipanga vyema na tayari vikosi vya wanyamapori vipo lindoni kupambana na Tembo waharibifu.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment