Image
Image

CLOUDS FM YATABNGAZA KUSAFIRISHA MWILI WA NGWEA KUTOKA AFRIKA KUSINI MPAKA HAPA TANZANIA.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam .


KAMPUNI ya Clouds FM, imejitolea kuusafirisha mwili wa marehemu Albert Mangwea kwa ajili ya kuutoa Afrika Kusini hadi Tanzania kwa ajili ya kuzikwa, ukiwa ni utaratibu unaoonyesha kuwa wadau wote wameamua kushirikiana katika suala hili.
Barua inayoonyesha walioanza kuchangia msiba wa Ngwea
Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds FM, Ruge Mutahaba, alithibitisha kuchukua uamuzi huo kwa ajili ya kufanikisha mazishi ya nyota huyo wa Bongo Fleva.
Taarifa za Kampuni hiyo kusaidia zilianza kuenea tangu juzi, baada ya Kamati ya Mazishi kushindwa kutaja makampuni, taasisi na watu walioanza kuchangia kwenye msiba huo.
Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba
"Tumeamua kwa mikono miwili kushiriki katika msiba huu wa ndugu yetu Mangwea,” alisema kwa ufupi.
 
Ngwea amepangwa kuletwa Tanzania kesho Jumamosi na kuagwa Jumapili, kabla ya kupelekwa mkoani Morogoro kwa ajili ya mazishi yake.
 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment