Image
Image

EXCLUSIVE: JB WA BONGO MOVIE AELEZEA MSIBA WA MANGWEA.

Wasanii wa bongo movie nchini Tanzania  wameungana na wasanii wezao wa muziki wa kizazi kipya katika kuomboleza kifo cha msanii maarufu Hip-hop Albert Mangwea  kilichotokea  nchini Afrika Kusini alikokuwa kikazi.

Akizungumza huku akionekana mwenye huzuni mwenyekiti mstaafu wa bongo movie Jacob Stephen maarufu kwa jina la JB amesema wameupokea msiba huo  kwa huzuni kubwa juu ya kufariki kwa msanii Albert Mangwea a.k.a. MIMI  kwa kuwa ameacha pengo kubwa kwa wasanii wa bongo fleva hususani wa miondoko ya hip-hop na Bongo fleva .
JACOB STEPHEN JB- MWENYEKITI MSTAAFU BONGO MOVIE
Kwaupande wake mayasa mrisho amesma ameguswa mno na msiba wa msanii huyo kikubwa ni kumuombea dua.

MAYASA MRISHO - MSANII WA BONGO MOVIE
MAREHEMU MANGWEA - KIPANDE HIKI NI KATIKA NGOMA ALIYOKUWA  WAMESHIRIKIANA KUIMBA NA FID Q

Katika kuonyesha kuguswa zaidi na msiba huo msanii wa muziki wa kizazi kipya Judith Wambura maaarufu kama lady JD ama lady anaconda ameshindwa kuzungumza na vyombo vya habari hali iliyomfanya Gadna G Habashi ambaye ni mume wa msanii huyo kuzungumzia juu ya uamuzi wa lady JD kuahirisha tamasha lake lililokuwa lifanyike tarehe 31 mwezi huu hadi hapo baadaye ili kuwapa nafasi wapenzi wake kuomboleza msiba huo.
GADNA HABASHI - MUME WA LAD JAYDEE.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment