Image
Image

SERIKALI: ATAYEHUJUMA MIUNDOMBINU YA MABOMBA YA GESI MTWARA KUKIONA CHA MOTO.



BOMBA la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam, linaanza kutandazwa leo likianzia mkoani Lindi. Kutokana na hali hiyo, Serikali imeonya kwamba, yeyote atakayethubutu kuharibu miundombinu ya bomba hilo, atachukuliwa hatua. 

Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alipofanya ziara ya kukag
ua, ubora wa vifaa, rasilimali watu na maandalizi ya miundombinu ya kutandaza bomba hilo. 


Wakati wa ziara hiyo ya siku moja, alikuwapo pia Balozi wa China nchini, Lu Youging, viongozi mbalimbali wa Serikali na viongozi wa kampuni zinazotandaza bomba hilo.



Profesa Muhongo alisema ameridhishwa na maandalizi yanavyokwenda, kwa kuwa kuna vifaa vya kisasa na imara.



Kesho kutwa (leo), utandazaji wa bomba unaanza rasmi na kwa maandalizi niliyoshuhudia, nina imani mradi huu utakamilika kabla ya Desemba mwaka 2014.



“Naomba Watanzania wawe na imani kubwa na watoe ushirikiano kwani utandazaji wa bomba utafanyika katika pande zote mbili, kwa maana ya nchi kavu na baharini.



“Mradi huu ni wa gharama kubwa na kama mnakumbuka, tulikopa fedha kutoka Benki ya Exim ambazo ni Dola za Marekani bilioni 1.2 kwa masharti nafuu.



“Pamoja na kwamba nia yetu ni nzuri, kuna baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya nchi hii, nataka kuwahakikishia Watanzania wote, kwamba usalama wa miundombinu hii utakuwa shwari na kama mtu anataka kushughulikiwa na Serikali, basi ajaribu kuihujumu atakiona cha mtema kuni.



“Hapa tumeshuhudia Watanzania 45 walioanza kupata ajira kama madereva, vibarua, kampuni za usafirishaji, huu ni mwanzo tu na ikifika sehemu ya kuhitaji watu wenye utaalamu, wataajiriwa wenye utaalamu,” alisema Profesa Muhongo.



Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mabomba yanayotandazwa ni ya aina mbili yakiwamo ya inchi 36 na uzito wa tani tano na yenye inchi 24 yakiwa na tani tatu ambayo alisema kwa ujumla wake yatadumu kwa miaka 30 na kama yakitunzwa vizuri yatadumu hadi miaka 70.



“Tunataka ifikapo mwaka 2016, tuwe na umeme wa megawati 3000 na mwingine wa ziada wa utakaokuwa ukiuzwa nje ya nchi ikiwamo Kenya ambayo imeleta maombi ya kuuziwa megawati 1000,

” alisema.

Pamoja na kufanya ziara hiyo juzi, Profesa Muhongo alisema itakuwa ni endelevu na itakuwa ikihusisha waandishi wa habari.



Naye, Balozi Youging, alisema gesi ni kitega uchumi kizuri ambacho kinaweza kuwaondoa Watanzania katika umasikini.



“China ni moja ya nchi iliyonufaika na gesi na ndio maana raia wake ni wataalamu wa nishati hiyo, naamini upatikanaji wa gesi hapa Tanzania, utasaidia Watanzania kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni.



Kwa upande wake, Meneja Mradi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, Mhandisi Baltazari Thomas, alisema hadi sasa watu 163 wamepata ajira katika awamu ya kwanza na kati ya hao Watanzania ni 68. 

MTANZANIA
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment