Image
Image

Bunge la Uganda lapiga marufuku kusafirishwa kwa wasichana na wanawake nchi za nje.




Bunge la Uganda limepitisha azimio la kupiga marufuku kuwasafirisha wasichana na wanawake wa nchi hiyo katika nchi za nje, ili kufanya kazi kama watumishi wa ndani, kufuatia kuwepo kwa matukio ya kufanyiwa ukatili na waajiri wao.

Katazo hilo linatokana na taarifa ya iliyowasilishwa bungeni na Waziri wa Nchi anayehusika na Wazee pamoja na Walemavu, Sulaiman Madada, iliyosema serikali inafahamu malalamiko
ya ukatili wananchi wa Uganda wanaofanyakazi za watumishi wa ndani katika nchi za Uarabuni.


Wakati wa mjadala wa hoja hiyo wabunge waliishutumu serikali kwa kuwatelekeza wananchi wa Uganda, wasio na matumaini ya ajira, na kujikuta wakitegemea ukarimu wa makampuni 24 yaliyosajiliwa kuwatafutia ajira nchi za nje.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment