Mbunge wa Kahama, Mheshimiwa JAMES LEMBELI amewataka wananchi wa Kahama na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la wapiga Kura baadae mwezi huu.
Amesema kujiandikisha kwenye daftari hilo ndiko kutawaweka tayari katika uchaguzi mkuu utakaowawezesha kuchagua viongozi bora wenye dhamira ya kweli ya kuwaongoza Watanzania.
Ameyasema hayo alipokuw akiwahutubia wananchi kwenye mkutano hadhara Mjini Kahama Mkoani Shinyanga.
Mheshimiwa LEMBELI amesema Tanzania bado inahitaji viongozi bora wanaozingatia maadili ya uongozi na kushirikiana na wananchi katika kuiletea maendeleo Tanzania na hivyo njia pekee itakayowezesha kupatikana kwa viongozi hao ni kwa wananchi wengi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Home
News
Lembeli awataka wananchi wa kahama na watanzania kujitokeza kujiandikisha katika Daftari la wapiga kura
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment