Image
Image

Serikali ya Mseto yaanza kunukia CCM

Mbarali.
Wapo wastaafu wengi wa Serikali ambao wanafuatilia kwa karibu nyenendo za siasa nchini, mmoja wapo ni Kanali Mstaafu Edmund Mjengwa (68) ambaye amekitahadharisha chama cha CCM kwamba kijiandae kwa Serikali ya mseto.

“Na endapo Rais atatoka CCM na wabunge wengi ndani ya Bunge wakawa ni wa upinzani, basi lazima Rais huyo akubali kufanya kazi na upinzani.

“Itabidi akubali kuunda Serikali ya mseto, japo sitarajii kufika huko. CCM ni imara, lakini tuwe na fikra hizo pia kwa nia nzuri ya kuiweka nchi katika amani,” ni kauli ya Kanali Mjengwa ambaye pia ni mkuu wa wilaya mstaafu.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili nyumbani kwake Mbarali, Kanali Mjengwa alisema licha ya upinzani kuwepo na kujipambanua kwa wananchi, lakini bado siyo tishio kwa CCM na itaendelea kushika dola tu kwani inaaminika na Watanzania wengi.

“Upinzani kuingia Ikulu bado sana, ila kwenye nafasi ya ubunge na udiwani ndiko kutakuwa na changamoto kubwa. Kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wengi wakatoka upinzani lakini siyo Rais.

“Lakini niseme tu kwamba pamoja na CCM kuendelea kuaminiwa na wananchi wengi, isibwete wala kupuuza upinzani. Hawa jamaa wanazidi kujitanua kweli kweli, hivyo wanaweza kuiyumbisha,” alisema Kanali Mjengwa.

Kanali Mjengwa alisema CCM bado inaaminiwa na Watanzania wengi, lakini tatizo linalomkera na mabalo kwa maoni yake linaharibu adabu na sifa ya CCM ni kitendo cha wana-CCM kuchafuana majukwaani.

Alisema CCM imetoka mbali na inatakiwa kuongoza kwa vitendo na siyo kupiga kelele za kuchafuana majukwaani kama ambavyo ilivyo hivi sasa.

Kwa mujibu wa Kanali Mjengwa anachukia  kuona mwana-CCM anatumia jukwaa kumchafua mwenzake kisa tu wote wametangaza nia ya kugombea nafasi fulani ya uongozi.

“Kama unona mwana CCM fulani amekwenda ndivyo sivyo kuna taratibu za vikao ndani ya chama, wakazungumzie na kumaliza tofauti hizo ndani ya Chama ili kulinda heshima ya Chama na si vinginevyo.

“Na kitendo hicho ndicho kinachowapa nguvu wapinzani kwa kusemea na kutunanga kwa Wananchi hatimaye CCM inaonekana kutokuwa na watu makini,” alisema.

Kanali Mjengwa alisema katika kuelekea uchaguzi mkuu hali ya kisiasa inazidi kupamba moto na kila chama kinazidi kujipambanua kivyake kwa wananchi kikitaka kuungwa mkono.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment