Image
Image

Japan yachangia sh. Milioni 160 shule ya msingi kakuni

Kaimu Balozi wa Japan, Bw. Kazuyoshi Matsunaga akisoma risala fupi mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia) wakati wa hafla fupi ya utiaji saini mkataba wa msaada wa shilingi milioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali ya Kakuni wilayani Mlele Machi 6, 2015 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam.(Picha zote na Zainul Mzige).
 Baadhi ya watendaji ofisi ya Waziri Mkuu waliohudhuria hafla hiyo fupi ya utiaji saini mkataba wa msaada na Ubalozi wa Japan wa shilingi milioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali ya Kakuni wilayani Mlele Machi 6, 2015 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dkt. Ibrahim Mzengi (wa kwanza kushoto) akiwa na watendaji wa mkoa wa Katavi na wilaya ya Mlele alioambatana nao kwenye hafla hiyo fupi. Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhandisi Kalobelo (wa pili kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Mlele, William Mwakalambile (wa pili kulia) pamoja na Afisa Mipango wa wilaya ya Mlele, Seif Mohamed Makome (kulia).
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akishuhudia tukio la kubadilishana hati za mkataba wa msaada baina ya Kaimu balozi wa Japan nchini, Kazuyoshi Matsunaga (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Mlele, William Mwakalambile (kulia).
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitoa neno la shukrani kwa Serikali ya Japan mara baada ya hafla ya utiaji saini wa mkataba wa msaada huo.
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifanya 'Power point presentation' ya hatua ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Kibaoni aliyoijenga kutokana na michango ya wadau wa maendeleo kama kurudisha fadhila kwa jamii yake iliyomsomesha kijijini kwake.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi wa Japan nchini, Kazuyoshi Matsunaga (kulia kwake) baada ya kushuhudia utiaji saini mkataba wa msaada wa Japan wa shilingi milioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Awali ya Kakuni wilayani Mlele Machi 6, 2015 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dkt. Ibrahim Mzengi na wapili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhandisi Kalobelo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele, William Mwakalambile.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment