Image
Image

Dr Slaa asema hakuna sababu serikali kutumia gharama kubwa sherehe za muungano huku wananchi wakiteseka hali ngumu ya maisha



Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Dokta Wilbrod Slaa amesema  hakuna sababu ya serikali  kutumia gharama kubwa kwenye  sherehe za muungano huku wananchi wakiendelea kuteseka kutokana na  ugumu wa maisha  na  kukosa  huduma muhimu   na  kuendelea kuelemewa na  mizigo mikubwa ya kodi  na michango  ya ujenzi wa maabara.
Dokta slaa ameyasema hayo mjini Morogoro wakati akihutubia  mamia ya wakazi wa manispaa ya Morogoro katika uwanja wa kiwanja cha Ndege ambapo amesema kudumisha muungano si kusherekea bali ni kufanya mambo ambayo yataweza kudumisha muungano huo na kusema kuwa lazima muungano  uwe wa serikali tatu ambapo amewataka wananchi wa mkoa wa morogoro kuunga mkono jitihada za ukawa kwa kupiga  kura ya hapana katiba inayopendekezwa.
Kuhusu maadhimisho ya siku ya wafanyakazi yaani Mei Mosi  yatakayofanyika kitaifa jijini Mwanza  ambapo  Dr Slaa amesema amealikwa lakini  haoni sababu ya kushiki kutokana na serikali  kupuuza madai ya msingi  na  haki za wafanyakazi  kwa muda mrefu  ambapo amewataka wafanyakazi kufanya maamuzi magumu  kuipa  nafasi serikali  itakayosimamia malalamiko ya wafanyakazi kwa vitendo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment