Image
Image

Mfungwa wa Palestina aliyeweka mgomo wa kutokula siku 55 kuachiwa majuma mawli yajayo.


Mfungwa wa Palestina aliyekuwa kwenye mgomo wa kula KHADER ADNAN,anatarajiwa kuachiwa katika kipindi cha majuma mawili yajayo.

Mwanasheria wa  Klabu ya Wafungwa  yenye makao yake Mjini Ramallah, Bwana JAWAD BOULOS amesema ADNAN amekubali kusitisha mgomo wa kula uliodumu kwa siku 55 na anatarjiwa kuachiwa tarehe 12 mwezi jao.

Bwana BOULOS amesema chini ya makubaliano yaliyofikiwa, Israel pia imeahidi kutomkamata tena Bwana ADNAN kwa kile kinachofahamika kama sheria ya kuwekwa kizuizini bila ya kufunguliwa mashitaka.

ADNAN  ameshikiliwa kwa miezi 11 chini ya sheria hiyo ambayo Israel inaitumia kuwazuia Wapalestina bila ya kuwafungulia mashitaka na hiyo ilikuwa ni mara yake ya tisa kuzuiliwa gerezani chini ya sheria hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment