Dereva wa gari lililokamatwa na fedha hizo Bw.
Rashidi Shabani Nkungu mkazi wa Dodoma amesema alikodishwa na watu watatu wenye
asili ya kiasia kutoka uwanja wa ndege kwenda Hoteli ya St. Gasper iliyoko mjini Dodoma.
Kwa upande wake meneja wa Hotel ya St. Gasper
Bw,Denis Johanes amesema alibaini kuwepo kwa
jambo lisilo la kawaida baada ya maelezo aliyompa wakati anatafuta
chumba kutofautiana na aliyoandika
kwenye kitabu cha wageni.
Alipotakiwa kueleza anakopeleka fedha hizo mtuhumiwa
huyo pamoja na kukiri kuwa yeye ni mfanyakazi wa kampuniya Quality Group
amesema alikuwa katika miamala yake ya kawaida.
Wakati jeshi la Poisi likiwa bado halijatoa
ufafanuzi,kukamatwa kwa fedha hizo zinazokadiriwa kufikia
zaidi ya milioni mia saba kumeongeza joto la wananchi na wana CCM wa
mkoa wa Dodoma la kutoridhishwa na mwenendo wa matokeo ya vikao vinavyoendelea.
0 comments:
Post a Comment