Image
Image

Diego Costa ashitakiwa.


Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa ameshtakiwa kwa madai ya kutaka kuzua ghasia ambayo hayakuonekana na maafisa wa mechi hiyo lakini ambayo yalinaswa katika ukanda wa video.
Mshambuliaji huyo alihusishwa katika kisa na beki wa Arsenal Laurent Koscielny katika dakika ya 43 ya mechi.
Mchezaji huyo ana hadi saa kumi na mbili hapo alhamisi jioni kujibu mashtaka hayo.
Naye Beki wa Arsenal Gabriel ameshtakiwa kwa utovu wa nidhamu kwa tabia yake wakati alipopewa kadi nyekundu huku Santi Carzola akionywa kuhusu tabia yake mbaya.
Wakati huohuo vilabu vyote viwili vimeshtakiwa kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji wake chini ya sheria za FA.
Vilabu vyote viwili pamoja na Gabriel vina hadi saa kumi na mbili jioni siku ya alamisi kujibu mashtaka hayo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment