Image
Image

Mahakama moja ya Ujerumani imewahukumu viongozi wawili wa waasi nchini Rwanda.

Mahakama moja ya Ujerumani imewahukumu viongozi wawili wa waasi nchini Rwanda kwa kupanga njama za kushambulia raia katika jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Ignace Murwanashyaka na Straton Musoni wanatuhumiwa kwa kuwaagiza wapiganaji kufanya mauaji ya halaiki pamoja na ubakaji kati ya mwaka 2008 na 2009.
Kesi yao ilifanyika chini ya sheria ambayo inaruhusu kuwashtaki wageni kwa uhalifu ulioyafanyika nje ya taifa la Ujerumani.
Hatua hiyo ilionekana kama ushindi dhidi ya waasi waliotekeleza uhalifu nchini Rwanda.
Murwanashyaka,ambaye ni kiongozi wa kikosi cha FDLR alipewa hukumu ya miaka 13 huku Musoni ambaye ni naibu wake akihukumiwa mika 8 jela.Hatahivyo Musoni ameachiliwa huru kutokana na miaka aliyokuwa akizuiliwa.
Uwepo wa FDLR mashariki mwa Congo ni moja ya maswala yanayosababisha mizozo ya miaka nenda miaka rudi nchini humo na kusababisha vifo vya watu milioni tano katika eneo hilo.
Wawili hao waliokamatwa ,mwaka 2009 wamekuwa wakiishi nchini Ujerumani tangu mapema miaka 1990 na kutoka huko walipanga mashambulizi dhidi ya raia mashariki mwa Congo.
Walishtumiwa kwamba waliagiza mauaji ya watu kwa kukataa kushirikiana na FDLR.
 Wakati wa kuanza wa kesi hiyo miaka minne iliopita,kiongozi wa mashtaka wa Ujerumani Christina Ritscher alisema kuwa wawili hao walikuwa wanajua kila kilichokuwa kikiendelea.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment