Image
Image

Hali ya Nsa Job si nzuri,vipimo vya baini fuvu lake limeathiriwa vibaya.

Uchunguzi wa mwanzo wa madaktari katika Hospitali ya KCMC mjini Moshi, unaonyesha Nsa Job ameumia sana.
Rafiki yake wa karibu ameiambia SALEHJEMBE kwamba bado hali ya kiungo huyo mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Coastal Union si nzuri.
“Walifanya kipimo cha CT Scan kuangalia kuhusiana na fuvu lake. Inaonekana limeumia sana kwa kweli na hali yake si nzuri,” alisema rafiki huyo.
Nsa alipigwa jiwe kubwa juzi usiku karibu na nyumba na Davis Mosha ambaye ni mgombea wa ubunge Moshi Mjini kupitia CCM.
Alikuwa akitokea kwa Mosha ambaye ni rafiki yake, watu wanaosadikiwa ni wafuasi wa Ukawa ndiyo walipiga jiwe lililopasua kioo cha gari alilokuwamo na kumjeruhi vibaya.
Jana Mosha aliiambia SALEHJEMBE kwamba wakati anakwenda nyumbani kwake alikuta watu hao wakiwa wameziba barabara na mawe makubwa.
Aliwasihi kuacha vurugu akisisitiza si jambo la busara, wakamsikiliza.
Lakini baadaye wakaanza kuwashambulia karibu kila mmoja aliyekuwa akipita katika barabara hiyo kwenda au kutoka kwake.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment