Image
Image

Barcelona wakiwa nyumbani wamechomoza na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya AS Roma.


Barcelona wakiwa nyumbani wamechomoza na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya AS Roma katika mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Bayern Munich wakiichapa Olympiakos mabao 4-0, Maccabi Tel Aviv wakilala hoi kwa Chelsea kwa kichapo cha mabao 4-0.

Arsenal walijiwekea hai matumaini ya kufuzu kwa hatua ya makundi kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Dinamo Zagreb.

BATE Borisov wakifungana bao 1-1 na Bayer Laverkusen, FC Porto wakilala 2-0 dhidi ya Dynamo Kiev, Zenit St P wakiichapa Valencia 2–0 na Lyon wakilala mbele ya KAA Gent bao 2-1.

Michuano hiyo inatarajia kuendelea tena hii leo kwa michezo kadhaa.

Miongoni mwa mechi hizo ni Man United dhdi ya PSV Eindhoven, Atletico Madrid na Galatasaray, Juventus dhidi ya Man City na Shakhtar Donetsk watawaalika Real Madrid.

Matokeo kamili ya mechi zilizochezwa ni kama ifuatavyo:

Barcelona 6 - 1 AS Roma

Arsenal 3 - 0 Dinamo Zagreb

Bayern Munich 4 - 0 Olympiakos

Maccabi Tel-Aviv 0 - 4 Chelsea

BATE Borisov 1 - 1 Bayer Leverkusen

FC Porto 0 - 2 Dynamo Kiev

Zenit St Petersburg 2 - 0 Valencia

Lyon 1 - 2 KAA Gent

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment