Image
Image

Malkia Elizabeth, Mfalme Akihito wampongeza JPM.

RAIS John Magufuli ameendelea kupokea salamu za pongezi kutoka kwa viongozi mbalimbali duniani kutokana na kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, safari hii akiwamo Malkia Elizabeth II wa Uingereza.
Katika salamu hizo, Malkia Elizabeth II amemueleza Dk Magufuli kuwa, “Natumaini kuwa uhusiano baina ya nchi hizi mbili ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Madola yataendelea wakati wa utawala wako, nakutakia heri pamoja na wananchi wa Tanzania.”
Mwingine aliyemtumia salamu Rais ni Mfalme Akihito wa Japan ambaye alimueleza Dk Magufuli, “Nakutumia salamu za dhati, mafanikio na furaha kwako Mheshimiwa Rais na watu wa nchi yako.”
Dk Magufuli pia amepokea salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Saharawi, Mohamed Abdelaziz aliyemtakia heri Rais na kumueleza kuwa “Nina imani kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea vyema chini ya uongozi wako kuelekea katika kupata maendeleo na mafanikio zaidi.”
Pia alikipongeza Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Watanzania kwa uchaguzi wa kidemokrasia ulioendeshwa katika mazingira ya kistaarabu chini ya usimamizi wa waangalizi kutoka kwenye kanda, bara na kimataifa na hivyo kuliletea sifa Bara la Afrika.
Aidha, amepokea salamu kutoka kwa Rais wa Namibia, Hage Geingob na kumueleza Rais kuwa salamu zake na zile za wananchi wa Namibia ni za dhati kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla kwa ushindi wa kiti cha urais.
Salamu kama hizo zimetoka kwa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye amesema Tanzania kwa mara nyingine tena imedhihirisha kuwa ni nguzo ya demokrasia barani Afrika. Naye Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Joachim Gauck alimtakia Dk Magufuli na Watanzania kwa ujumla mafanikio katika kuendeleza Taifa kwa ujumla.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment