''Suala la mapambano dhidi ya ugaidi ni moja kati ya maswala muhimu,hasa baada ya matukio mabaya kama utekaji nyara na vifo vilivyotokea nchini Ufaransa, kama tunavyoelewa na imekuwa ikizungumzwa kabla, kuwa njia za ufadhili wa fedha kwa ajili ya vitendo vya kigaidi vikomeshwe,nimetoa mifano kwa taarifa tulizonazo kuhusu watu kutoka nchi mbalimbali wanaotoa ufadhili kwa wanamgambo wa IS, tumebaini kuwa ufadhili huu unatoka nchi 40 zikiwemo baadhi za G20''. Alieleza Putin.
Nae Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema kuwa mashambulizi ya Paris yalikuwa yakipangwa nchini Syria lakini yaliandaliwa nchini Ubelgiji.Wapelelezi wanashuku kuwa mtu aliyekuwa anasuka mipango hiyo ni Abdelhamid Abaaoud, mwenye miaka 27, mbelgiji mwenye asili ya morocco, anatoka katika wilaya ya Molenbeek.
Polisi nchini Ubelgiji wamewashutumu watuhumiwa wawili na wanamtafuta Salah Abdeslam, raia wa ufaransa aishie mjini Brussels ambaye nduguye anaaminika kuwa alijitoa muhanga mjini Paris.


0 comments:
Post a Comment