Image
Image

Jaji Mutunga aishauri Serikali ya Tanzania kuharakisha upatikanaji wa katiba mpya.

Jaji Mkuu wa Kenya Dokta Willy Mutunga ameishauri Serikali ya Tanzania kuharakisha mchakato wa Katiba Mpya iliyopendekezwa  ili itoe fursa kwa mahakama nchini kufanya kazi zake kwa uwazi na weledi pamoja na kuwashirikisha wananchi hasa katika uteuzi wa majaji wakuu.
Amesema, ili hilo litekelezwe kwa ufanisi Katiba pekee ndiyo jibu la kuleta maendeleo katika Nyanja zote kwani itaweza kuzingatia masilahi ya Watanzania na nchi kwa ujumla.
Jaji Mutunga ameyasema hayo wakati wa mazungumzo maalumu na vyombo vya habari mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na mwenyeji wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Chande Othman Chande katika Mahakama  Kuu ya Tanzania. Jijini Dar es salaam.
Katika mazungumzo yao yenye lengo la kubadilishana uzoefu wa kimahakama, ni pamoja na mabadiliko ya Katiba ya Kenya, Uhusiano wa Mahakama na Wananchi ambapo Jaji Mutunga amesema, uteuzi wa Majaji wakuu nchini mwake sasa unashirikisha wananchi tofauti na awali ambapo Katiba ilikuwa ikikiuka.
Kuhusu Kurejewa tena kwa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya, Dk Mutunga amesema itatoa fursa kwa mahakama nchini kufanya kazi zake kwa uwazi na weledi pamoja na kuwashirikisha wananchi hasa katika uteuzi wa majaji wakuu.
Pamoja na Kila nchi kuwa na utaratibu wake katika mihimili mikuu ya Serikali Jaji Chande Othman Chande amekiri kuongezwa uwazi zaidi kwa wananchi huku akianisha baadhi ya hatua za kuteua majaji wakuu nchini.
Ziara ya Jaji Mkuu huyo wa Kenya imekuja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya sheria ambayo yanafikiwa kilele Alhamisi hii, huku mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Rais wa Tanzania Dk Magufuli.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment