Image
Image

Maafisa nchini Marekani kuchunguza virusi vya Zika kuenezwa kwa njia ya ngono.

Maafisa wa afya nchini Marekani wanachunguza taarifa nyingine 14 za uwezekano wa kuenezwa kwa virusi vya Zika kwa njia ya ngono. 
Visa hivyo vinahusisha wanawake kadhaa wawajawazito, kilieleza kituo cha CDC.
Kituo cha Marekani cha udhibiti wa magonjwa (CDC) kimefichua hayo wakati kikizindua muongozo mpya juu ya maambukizi ya virusi hivyo kwa njia ya ngono . 
Muongozo huo umetolewa kufuatia kuthibitishwa kwa kisa cha kwanza cha Zika kwa mtu ambae hakusafiri nchini Marekani.
Kisa hicho kilikuwa na uhusiano na tendo la kujamiiana na mpenzi alieambukia virusi vya Zika.
Kituo cha CDC kinawashauri wanaume wote ambao wamesafiri kwenye maeneo yenye virusi vya Zika kutumia mipira ya kondomu ama kuacha kufanya tendo la ngono kwa kipindi cha ujauzito.
Hakuna ushahidi bado kwamba wanawake wanaweza kueneza virusi vya Zika kwa wapenzi wao, lakini utafiti zaidi unahitajika kuelewa suala hili, kilieleza kituo hicho cha afya ya mwili.
Njia kuu ya maambukizi ya Zika kwa sasa bado ni kuumwa na mbu.
Wataalam wanasema wanawake wajawazito wanapaswa kujaribu kuepuka kuumwa na wadudu.
Jumanne, Margaret Chan, mkuu wa Shirika la Afya Duniani, alisema kuwa dunia inakabiliwa na "safari ndefu "ya kutokomeza Zika.
Akizungumza nchini Brazil, ambako visa vingi vimeripotiwa, alisema kuwa "virusi vya Zika ni vigumu, na itahitaji ujuzi wa hali ya juu " kuviangamiza.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment