Image
Image

Serikali yawataka wananchi kutumia masanduku kutoa maoni juu ya huduma za Afya.


Serikali imewataka wananchi wanaopata huduma mbalimbali za afya ya mama na mtoto katika hosipitali,vituo vya afya na zahanati za umma kutumia masanduku ya maoni kutoa malalamiko yao pale wanapoona hawajatendewa haki na watoa huduma ili hatua dhidi yao zichukuliwe na kukomesha ukiukwaji wowote wa haki za mteja.
Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mhe. Hamis Kigwangala ametoa wito huo kwa wananchi wakati akijibu swali lililoulizwa na mbunge wa viti maalum Faida Mohamed Bakar aliyehoji kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa huduma na haki za afya ya uzaji katika maeneo mbalimbali nchini na kuhatarisha maisha ya wanawake.
Naibu waziri Kigwangwala amesema katika kutekeleza suala hilo serikali itaweka na kusimamia masanduku ya maoni katika sehemu zote za kutolea huduma za afya ili wananachi wapate fursa ya kutoa maoni yao kwa mtoa huduma yetote atakayekiuka haki za mteja na kuchukuliwa hatua.
Mhe.Kigwangwala ameongeza kwa kuesema kuwa mazoezi ya ukaguzi na ufuatiliaji wa kushtukiza yanayofanywa na kiongozi yeyote wa serikalini mwenye dhamana ya kusimamia huduma za jami katika vituo vya kutolea huduma za afya vya umma na binafsi tayari yameanza kuzaa matunda kwenye uboreshaji wa huduma na haki kwa wateja kwenye sekta hiyo


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment