Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh.Charles Kitwanga
amewataka wananchi visiwani Zanzbar kuondokana na hofu ya kuwepo askari wengi
katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa marudio kwani
wapo kwa ajili ya kuimarisha amani na usalama wao.
Akizungumza na wananchi alipokuwa akitembelea katika maeneo
mbali mbali ya kisiwani Pemba waziri huyo amesema amepata faraja ya kuwa
wananchi wanaendelea na shughuli zao vizuri bila ya kubugudhiwa huku akikanusha
taarifa za kuwepo kwa watu waliojificha katika misitu wakikimbia askari.
Mh.Kitwangwa aliwaagiza msafara umpeleke msitu mkuu
wangezi ambapo aliambiwa kunawatu wamekimbilia huko na mara baada ya kufika
alimtaka kamanda wa polisi mkoa Kaskazini na mkuu wakituo konde kuonyeshwa watu
hao nakugundua kuwa hakuna ukweli juu ya uwepo wa watu hao na kuwataka
watu kuacha kauli za kuwafanya watu waogope kuwa kunatatizo kumbe hakuna.
Baadae alitembelea kambi zilizofikia askari katika kambi ya
FFU Mfikiwa mkoa kusini Pemba na FFU mkoa kaskazini Pemba ambapo mkuu wa mkoa
kusini Pemba aliwataka askari waliopo kwenye makambi hayo kufanya kazi kwa
uwadilifu ilikuhakikisha watu wanapiga kura pasi na kubughudhiwa.
0 comments:
Post a Comment