Watu wa wili akiwemo Dereva wamefariki dunia wengine
kujeruhiwa baada ya Bus la Leina Tours lililokuwa likitokea KAHAMA kwenda DSM kupoteza
Mwelekeo wakati likitaka kukwepa gari ndogo na kuingia Mtaro wa maji ya mvua
Kimara Bucha jijini Dar es Salaam.
Ajali hiyo ambayo imetokea usiku wa kuamkia leo
imezua taharuki kwa wakazi wa eneo hilo la Kimara Bucha ambapo wengi wao
walionekana kuduwaa huku wakishindwa kuelwa haswa mazingira kamili ya ajali.
Wananchi walionekana kufika msaada kwa manusura wa
ajali na walio poteza kuwapa msaada licha ya msemo wa kufa kufaana kutokuisha
baada ya watu wanaoonekana kuwa vibaka kuokoa huku wakiiba vitu.
Da poleni sana Madereva muwe makini tu mkumbuke mmebeba roho za watanzania na wasio watanzania.
ReplyDelete