Image
Image

Waziri Kairuki atoa siku moja tu kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma ujiji kumpa maelezo ya matumizi ya Bilioni 2.46.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora,ANGELA KAIRUKI ametoa siku moja kwa  mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji na mkoa kwa jumla kutoa maelezo ya matumizi ya shilingi BILIONI 2.46 zilizotolewa na serikali katika mwaka wa fedha 2014/2015 kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa nyumba za walimu, vyoo na usimamizi .
Ametoa maagizo hayo baada ya kamati ya bunge ya utawala bora na serikali za mitaa kutembelea shule ya sekondari kirugu kata ya majengo mjini Kigoma  na kukagua baadhi ya vyumba vya madarasa vilivyojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF awamu ya pili ambapo ilibainika kuwa shule hiyo haina nyumba za walimu, jingo la utawala, umeme na vyoo havitoshelezi.

Amesema hali hiyo inaonyesha jinsi fedha zilizotolewa na serikali hazikutumika kwa malengo yaliyokusudiwa katika mkoa wa Kigoma na kutaka taarifa hiyo iwasilishwe haraka kwa Waziri wa TAMISEMI - GEORGE SIMBACHAWENE
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment