Image
Image

Marehemu PAPA WEMBA aagwa Kinshasa, Kuzikwa eneo la Matongee siku ya Jumatano.

Leo Rais wa JAMHURI YA WATU WA CONGO JOSEPH KABILA ametoa nishani Maalum ya heshima kwa Mwanamziki nguli wa nchi hiyoJules Shungu Wembadio Pene Kikumba (PAPA WEMBA) aliefariki dunia jumapili iliyopita nchini Ivory coast wakati akitumbuiza.
Tuzo hiyo ametoa katIka ukumbi wa BUNGE LA nchi hiyo ulipo kwenye mjii mkuu wa KINSHASA  ambako Mwili wa Mwanamziki huyo  uNaagwa kwa heshima maalum ya Serikali na wabunge.
Siku ya leo  jumanne mwili wa PAPA WEMBA unapelekwa kwenye eneo la matongee eneo ambalo aliishi akiwa mtoto na wananchi watapata nafasi ya kuuga na kuzikwa siku ya jumatano hapo hapo jijini KINSHASA.
Maelfu ya waombolezaji wamefurika kuadhimisha misa ya wafu kwa heshima ya mwanamuziki nyota wa
muziki wa Soukus na Rhumba raia wa Jamhuri ya Congo Papa Wemba.
Waomboloezaji walipiga foleni ilikupata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa msanii huyo nguli aliyeaga dunia juma lililopita alipokuwa akiwatumbuiza mashabiki wake huko Abidjan Ivory Coast.
Mwili wake umewekwa katika majengo ya bunge mjini Kinshasa.
Serikali imetangaza siku tatu za maombolezi kuanzia leo hadi jumatano atakapozikwa.
Msanii huyo nguli a
likonga nyoyo za wapenzi wa muziki wa Soukus nchini DRC na kote duniani kwa kipaji chake cha kipekee na sauti isiyokuwa na mfano.
Wengi waliitambua sauti hiyo ya na utunzi wake.
Alikuwa ni mtumbuizaji kamili.
Gwiji huyo wa muziki wa Lingala alizaliwa mnamo Juni 14 mwaka 1949, katika eneo la Lubefu - Wilaya ya Sankuru nchini Congo.
Yeye alianza kazi ya muziki akiwa na umri mdogo mno.
Alikuwa akimfuata m
amake katika matanga na hivyo akaibukia kuwa mtunzi wa nyimbo za kuomboleza.
Mfalme huyo wa muziki wa Rhumba, mwenye umri wa miaka 66 aliaga dunia ghafla 24 April akiwa nchini Ivory Coast.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment