Image
Image

Simba yaitafuna Mbao Shamba la bibi jijini Dar es Salaam.

SIMBA jana ilizidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya kuifunga Mbao FC bao 1-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Ushindi huo umeifanya Simba kufikisha pointi 26 katika mechi 10 ilizocheza, ikiongoza kwa tofauti ya pointi sita dhidi ya Stand United iliyo nafasi ya pili na pointi 20.
Hata hivyo Simba ililazimika kupata bao hilo ‘jioni’ mwa mchezo huo kwani Mbao waliwabana kuanzia mwanzo wa mchezo na kama washambuliaji wake wangekuwa makini, wangevunja mwiko kwa kuwafunga vinara hao. Jana hakuwa Shizza Kichuya tena wala Ibrahim Ajib waliozoeleka kuipa Simba mabao, bali kazi hiyo ilifanywa na Mzamiru Yassin katika dakika ya 88.
Mzamiru alifunga bao hilo baada ya kuunganisha pasi ya Fredrick Blagnon na kuzusha shangwe kwa mashabiki wa Simba ambao walionekana walikwishakata tamaa ya kupata pointi zote tatu. Kwa ujumla Mbao iliisumbua Simba katika mechi hiyo ikionekana kuwashambulia huku ikiwa imekamilika kila idara.
Dakika ya 17 ya mchezo huo Simba ilikosa mabao kupitia kwa washambuliaji wake Laudit Mavugo, Kichuya na Ajib ambao mabeki wa Mbao walihakikisha hawachezi nao mbali ili wasilete madhara langoni mwao.
Mzamiru nusura aiandikie Simba bao katika dakika ya 21 lakini mpira aliopiga ulipaa juu ya goli. Dakika moja baadaye Hussein Swedi wa Mbao akatengeneza nafasi ya kwanza ya bao lakini akashindwa kujiamini na mabeki wa Simba wakaunasa mpira na kuuondoa kwenye eneo la hatari.
Kwa matokeo hayo, Mbao inayocheza Ligi Kuu kwa mara ya kwanza imebaki katika nafasi ya nane kwenye msimamo ikiwa na pointi 12 katika mechi 11 ilizocheza.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment