Image
Image

Maradhi ya saratani kuathiri wanawake zaidi miaka ya mbeleni

Kwa mujibu utafiti uliofanyika umedhihirisha kuwa kwanzia mwaka 2030 kila mwaka wanawake takriban milioni 5.5 watafariki kila mwaka kutokana na maradhi ya saratani.Ripoti ya utafiti kuhusu ugonjwa huo iliwasilishwa na shirika la American Cancer Society katika Kongamano la mwaka huu kuhusu maradhi ya saratani liliondaliwa jijini Paris nchini Ufaransa lilibainisha kuwa waathirika wengi wa maradhi haya wapo katika nchi zenye mapato ya chini na nyuma kiuchumi.
Katika ripoti hiyo imeonyesha pia kuwa na ongezeko la vifo,ongezeko la idadi ya wazee,matatizo ya unene na pia ukosefu wa lishe bora .
Vile vile ripoti hiyo imebainisha kuwa wanawake wanaathiriwa zaidi na ugonjwa wa saratani.
Kulingana na utafiti ulioonyeshwa katika ripoti hiyo mnamo mwaka 2012 watu milioni 8 walifariki kutokana na saratani na kati yao milioni 3.5 walikuwa wanawake .
Wanawake 1.7 wamefariki kutokana na saratani ya matiti .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment