Image
Image

Ziara ya kiserikali kukamilisha mikataba ya ushirikiano kati ya Kuwait na Tanzania.

BALOZI wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem, amesema nchi yake imeandaa ziara ya kiserikali kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk Augustine Mahiga, kuitembelea nchi hiyo ili kukamilisha mikataba ya ushirikiano kati ya nchi hiyo na Tanzania. Balozi Al Najeem alisema hayo kwenye hafla aliyoiandaa kwa ajili ya kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutimiza mwaka mmoja. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mabalozi wa nchi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania.
Alisema tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani imeimarisha ushirikiano na Kuwait kwa kuanzisha ubalozi wa nchini humo na kuwepo kwa balozi kumerahisisha na kuhamasisha wawekezaji wa Kuwait kuja kuwekeza Tanzania na wafanyabiashara kuleta bidhaa zao na kuagiza bidhaa za kilimo kupata soko nchini Kuwait.
Mikataba inayokusudiwa kusainiwa wakati wa ziara ya Waziri Mahiga nchini humo, itahusu ushirikiano katika nyanja ya uchumi ikiwemo wa kutotoza kodi mara mbili kwa bidhaa zinazoingia katika nchi hizi mbili, kukuza kiwango cha biashara na kusaidia sekta huduma za kijamii.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi Mahiga ameipongeza Kuwait kwa misaada ya kibinadamu na ya kiuchumi kwa Tanzania na kusisitiza kuwa Kuwait inastahili heshima ya kuwa kituo cha misaada ya kiutu duniani.
Aidha, aliishukuru kwa kuitikia haraka mwito wa kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera, Septemba mwaka huu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment