Image
Image

Chukueni Tahadhari na Matapeli wa M-PESA.

Ikiwa wateja mbalimbali wa Vodacom Tanzania wakiendelea kunufaika na bonasi za M-PESA zinazotolewa na kampuni hiyo,Kumetokea na matapeli wakiwalaghai wateja wa kampuni hiyo kana kwamba ni washindi wa bonasi hizo zinazoendelea kutolewa.
Vodacom Tanzania imetoa tahadhari kwa wateja wake wote popote walipo nchini kuwa macho na matapeli ambao wanajifanya ni wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa kuwapigia simu na kuwafahamisha kuwa wamefanikiwa kupata mgao wa fedha za gawio la huduma ya M-Pesa uliotangazwa na kampuni mapema wiki hii.
”KAMA WANAVYOSIKIKA KWENYE SAUTI HIYO”
Akiongea na Mtandao huu,Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu alisema“Natoa wito kwa wateja wetu kuwa makini na matapeli wanaowapigia simu na kuwafahamisha kuwa wameshinda fedha za bonasi ya M-Pesa.
Vodacom Tanzania haina utaratibu wa kuwapigia simu wateja kuhusiana na mgao wa fedha hizi bali inatoa mgao kwa kadri  ya mteja alivyotumia huduma hii na rekodi zote za matumizi kampuni inazo. Wanaowapigia simu wateja ni matapeli ambao wanataka kupata namba zenu za siri na kuwatajia kiasi gani cha fedha mlizonazo ili wapate frusa ya  kuwaibia fedha na msitoe namba   za siri kwa mtu yeyote”.
Wateja watakaonufaika na mgao wa fedha za bonasi ya M-pesa awamu hii wanawekewa fedha zao kwenye akaunti zao za M-Pesa moja kwa moja na utaratibu wa kuwapigia wateja simu huwa unatumika kwenye promosheni tu kama vile promosheni inayoendelea ya”Nogesha Upendo”.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment